Saturday, August 18, 2012

SIMBA BINGWA MICHUANO YA ABC SUPER8 KWA KUICHAPA MTIBWA SUGAR 4-3

Kikosi cha timu ya Simba B ambacho kilishuka dimbani hii leo katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam kumenyana na Mtibwa Suger ya turiani katika fainali za ABC Super8 Cup 2012 na kuwakimbiza wakata Miwa hao wa turiani kwa magoli 4-3. 

Simba iliwalazimu kutumia dakika 120 kuwararua wakata Miwa hao walikuwa wabishi kuwadhibiti Simba hao watoto walio kuwa wakiwatimua kila mara na mapanga yao ya kukatia miwa. 

Kwa matokeo hayo sasa Simba inakuwa timu ya kwanza kunyakua kombe hilo kwani ndio mara ya kwana kushindaniwa hapa nchini. simba pia iliwatoa Azam FC katika michuano ya Bank ABC Super8 nusu fainali kwa goli  2-1 katika mchezo huo.
waziri akikabidhi kombe kwa  nahodha wa simba Edward Christopher
waziri wa habari,vijana,utamaduni na michezo Mh Dk.Fenella Mkangala akiwakabidhi wachezaji medali wachezaji wa simba
wachezaji wakishangilia ushindi
mwenyekiti wa simba sc Ismail Aden Rage akiwapungia mashabiki baada ya ushindi
wachezaji wakiwa wamembeba kocha wao Suleiman Matola baada ya ushindi
wachezaji wa yanga wakishangilia ushindi

picha ya pamoja

No comments:

Post a Comment